,

Neno Quotes

Quotes tagged as "neno" Showing 1-4 of 4
Enock Maregesi
“Musa alipokuwa mlimani kupokea Amri Kumi za Mungu kwa ajili ya Wana wa Israeli alikawia sana kurudi, kiasi cha watu kukata tamaa na kujiona wapweke wakiwa njiani kuelekea katika Nchi ya Ahadi. Kutokana na woga usio na kifani na kukata huko kwa tamaa waliamua kutosubiri tena kusikia neno kutoka kwa Mungu, au kuiona sura halisi ya Mungu kama Musa alivyokuwa amewaahidi, hivyo wakamlazimisha Haruni awatengenezee mungu kutokana na taswira ambayo tayari walishakuwa nayo vichwani mwao kuhusu mungu waliyemtaka; yaani ndama wa dhahabu, au mungu mpya ambaye angewapa chochote walichotaka muda wowote waliotaka.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kwa nini mtoto mchanga anapokuwa ananyonya ziwa la mama yake, mara nyingi humwangalia mama yake machoni? Kwa sababu, licha ya macho kuonekana kitu cha ajabu kwake, mtoto mchanga, bila kujitambua, hutamani sana mama yake amwambie neno zuri atakalolitumia baadaye katika maisha yake atakapokuwa mkubwa. Maneno huumba. Ukimwambia mwanao kuwa anaonekana atakuwa jambazi, anaweza kuwa jambazi kweli atakapokuwa mkubwa; ukimwambia kuwa anaonekana atakuwa mwanasheria, anaweza kuwa mwanasheria kweli atakapokuwa mkubwa.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Jicho ni kiungo cha ajabu zaidi kuliko viungo vyote katika mwili wa mwanadamu baada ya ubongo. Jicho moja linatengenezwa na viungo vidogovidogo zaidi ya milioni mbili, vinavyofanya kazi kwa pamoja bila kukosea. Macho yana nguvu ya ajabu. Huu ni wito kwa akina mama wanaonyonyesha: Usizungumze maneno mabaya mtoto wako mchanga anapokuangalia machoni wakati ananyonya ziwa lako. Neno lolote utakalomwambia, zuri au baya, pamoja na kwamba amekuwa akisikia sauti yako kwa miezi kadhaa akiwa tumboni, litajirekodi katika akili yake isiyotambua bila wewe au yeye mwenyewe kujua. Neno hilo litakuja kumuathiri baadaye atakapokuwa mkubwa. Atakapopevuka, atakapokuwa na uwezo wa kupambanua mambo, atakuwa anaota na kuwaza kile ambacho ulikuwa ukimwambia alipokuwa tumboni; na alipokuwa akinyonya na kukukodolea macho.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mtu akisema neno usimfuatilie yeye, bali fuatilia neno alilolisema.”
Enock Maregesi
tags: neno, word