,

Asia Australia Quotes

Quotes tagged as "asia-australia" Showing 1-2 of 2
Enock Maregesi
“Meja Jenerali U Nanda, 60, Kiongozi wa Kanda ya Asia-Australia ya Tume ya Dunia ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya, alizaliwa Jumamosi ya tarehe 19/03/1932 kandokando ya mto huko Maubin nchini Bama. Yeye na familia yake ni waumini wa dini ya Ubuda. Mke wake, Daw Aung Phyu, ana miaka 57. Alizaliwa Jumapili ya tarehe 20/10/1935. Nanda na Aung Phyu wana watoto watatu. Ko Mahn Thiri (wa kiume na wa kwanza kuzaliwa) ana miaka 37. Alizaliwa Alhamisi ya tarehe 08/12/1955. Yeye na familia yake wanakaa nchini Tailandi. Ma Nang Nyi ni mtoto wa pili wa familia ya Nanda na Aung Phyu. Alikufa kwa madawa ya kulevya Jumamosi ya tarehe 12/05/1980 akiwa na miaka 23. Alizaliwa Jumamosi ya tarehe 06/04/1957. Miaka miwili baadaye mpenzi wake wa kiume, Ko San Pe, alikufa kwa madawa ya kulevya pia Jumatano ya tarehe 21/07/1982 akiwa na miaka 25. Alizaliwa Jumanne ya tarehe 29/01/1957. Ma Thida Wai Aung ni wa mwisho kuzaliwa. Ana miaka 34. Alizaliwa Jumatano ya tarehe 23/07/1958. Anakaa Rangoon na mume wake wa miaka sita na watoto wawili, wa kike na wa kiume. Saw Saya (Mkurugenzi wa Sekretarieti ya Kanda ya Asia-Australia ya Tume ya Dunia ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya, kutoka katika kabila la Karen) ndiye aliyempa taarifa U Nanda za kikao cha dharura cha Tume ya Dunia. Ana miaka 54. Alizaliwa Jumanne ya tarehe 01/03/1938.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Sanjay Kanaka Ramachandra, 'The Satellite', baada ya kutoka Korea ya Kaskazini na Salina Cruz kwa ajili ya kozi maalumu ya ugaidi na kwa ajili ya Kiapo cha Swastika kwa mpangilio huo, alirudi Mumbai kusimamia shughuli za Kolonia Santita za bara la Asia na Australia – kwa uaminifu wa Sheria ya Kitalifa ya Kolonia Santita. Ramachandra, anayeitwa 'The Satellite' kwa sababu ya jina lake la mwisho, alipewa pia jukumu la kuyachunga Makao Makuu ya Kanda ya Asia-Australia ya Tume ya Dunia; na kupeleka taarifa yoyote ya kijasusi (inayohusiana na WODEC-Rangoon) Mexico City kwa ajili ya maamuzi ya Mkurugenzi wa Usalama wa Kolonia Santita Gortari Manuel. Mojawapo ya operesheni kubwa alizowahi kuzifanya Ramachandra kwa niaba ya Kolonia Santita ni kuingiza nchini India mzigo wa tani 350 za majani ya koka, ijapokuwa tani 37 zilikamatwa na mamlaka za kuzuia madawa ya kulevya za India na za Tume ya Dunia, na kusambaza kilo 560 za kokeini safi (isiyokuwa na doa) katika nchi zote za Asia na Australia ndani ya siku 14.”
Enock Maregesi