,

Spear Quotes

Quotes tagged as "spear" Showing 1-16 of 16
“YOUR GREATER ANIMAL


They say that if you are
Ever confronted by
A lion or bear,
To never act scared.
Instead act like
You are the greater animal
And that they're
The hare
That you are about
To tear.
This has been
Proven
And compared.
This is how presidents
Are loved
And feared.
Each one of us has an animal
Within us
That is armed with
Mental,
Physical or
Spiritual gifts
That could shoot spears
Through the air.

So next time
You are confronted in
A fight that seems unfair,
Just remember the lion and the bear.
MAGNIFY
Your greater animal
And all that feel your magnificence
Will quickly step away
And disappear.”
Suzy Kassem, Rise Up and Salute the Sun: The Writings of Suzy Kassem

Enock Maregesi
“Biblia pamoja na historia vinatwambia kuwa mitume kumi na wawili wa Yesu Kristo waliamua kufa kinyama kama mfalme wao alivyokufa, kwa sababu walikataa kukana imani yao juu ya Yesu Kristo.

Mathayo alikufa kwa ajili ya Ukristo nchini Ethiopia kwa jeraha lililotokana na kisu kikali, Marko akavutwa na farasi katika mitaa ya Alexandria nchini Misri mpaka akafa, kwa sababu alikataa kukana jina la Yesu Kristo.

Luka alinyongwa nchini Ugiriki kwa sababu ya kuhubiri Injili ya Yesu Kristo katika nchi ambapo watu hawakumtambua Yesu.

Yohana alichemshwa katika pipa la mafuta ya moto katika kipindi cha mateso makubwa ya Wakristo nchini Roma, lakini kimiujiza akaponea chupuchupu, kabla ya kufungwa katika gereza la kisiwa cha Patmo (Ugiriki) ambapo ndipo alipoandika kitabu cha Ufunuo. Mtume Yohana baadaye aliachiwa huru na kurudi Uturuki, ambapo alimtumikia Bwana kama Askofu wa Edessa. Alikufa kwa uzee, akiwa mtume pekee aliyekufa kwa amani.

Petro alisulubiwa kichwa chini miguu juu katika msalaba wa umbo la X kulingana na desturi za kikanisa za kipindi hicho, kwa sababu aliwaambia maadui zake ya kuwa alijisikia vibaya kufa kama alivyokufa mfalme wake Yesu Kristo.

Yakobo ndugu yake na Yesu (Yakobo Mkubwa), kiongozi wa kanisa mjini Yerusalemu, alirushwa kutoka juu ya mnara wa kusini-mashariki wa hekalu aliloliongoza la Hekalu Takatifu (zaidi ya futi mia moja kwenda chini) na baadaye kupigwa kwa virungu mpaka akafa, alipokataa kukana imani yake juu ya Yesu Kristo.

Yakobo mwana wa Zebedayo (Yakobo Mdogo) alikuwa mvuvi kabla Yesu Kristo hajamwita kuwa mchungaji wa Injili yake. Kama kiongozi wa kanisa hatimaye, Yakobo aliuwawa kwa kukatwa kichwa mjini Yerusalemu. Afisa wa Kirumi aliyemlinda Yakobo alishangaa sana jinsi Yakobo alivyolinda imani yake siku kesi yake iliposomwa. Baadaye afisa huyo alimsogelea Yakobo katika eneo la mauti. Nafsi yake ilipomsuta, alijitoa hatiani mbele ya hakimu kwa kumkubali Yesu Kristo kama kiongozi wa maisha yake; halafu akapiga magoti pembeni kwa Yakobo, ili na yeye akatwe kichwa kama mfuasi wa Yesu Kristo.

Bartholomayo, ambaye pia alijulikana kama Nathanali, alikuwa mmisionari huko Asia. Alimshuhudia Yesu mfalme wa wafalme katika Uturuki ya leo.
Bartholomayo aliteswa kwa sababu ya mahubiri yake huko Armenia, ambako inasemekana aliuwawa kwa kuchapwa bakora mbele ya halaiki ya watu iliyomdhihaki.

Andrea alisulubiwa katika msalaba wa X huko Patras nchini Ugiriki. Baada ya kuchapwa bakora kinyama na walinzi saba, alifungwa mwili mzima kwenye msalaba ili ateseke zaidi. Wafuasi wake waliokuwepo katika eneo la tukio waliripoti ya kuwa, alipokuwa akipelekwa msalabani, Andrea aliusalimia msalaba huo kwa maneno yafuatayo: "Nimekuwa nikitamani sana na nimekuwa nikiitegemea sana saa hii ya furaha. Msalaba uliwekwa wakfu na Mwenyezi Mungu baada ya mwili wa Yesu Kristo kuning’inizwa juu yake." Aliendelea kuwahubiria maadui zake kwa siku mbili zaidi, akiwa msalabani, mpaka akaishiwa na nguvu na kuaga dunia.

Tomaso alichomwa mkuki nchini India katika mojawapo ya safari zake za kimisionari akiwa na lengo la kuanzisha kanisa la Yesu Kristo katika bara la India.

Mathiya alichaguliwa na mitume kuchukua nafasi ya Yuda Iskarioti, baada ya kifo cha Yuda katika dimbwi la damu nchini India. Taarifa kuhusiana na maisha na kifo cha Mathiya zinachanganya na hazijulikani sawasawa. Lakini ipo imani kwamba Mathiya alipigwa mawe na Wayahudi huko Yerusalemu, kisha akauwawa kwa kukatwa kichwa.

Yuda Tadei, ndugu yake na Yesu, aliuwawa kwa mishale alipokataa kukana imani yake juu ya Yesu Kristo.

Mitume walikuwa na imani kubwa kwa sababu walishuhudia ufufuo wa Yesu Kristo, na miujiza mingine. Biblia ni kiwanda cha imani. Tunapaswa kuiamini Biblia kama mitume walivyomwamini Yesu Kristo, kwa sababu Biblia iliandikwa na mitume.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Lakini damu na maji vina maana kubwa katika maisha yetu. Biblia inaeleza kuwa wakati Yesu Kristo akiwa msalabani alichomwa ubavu wake kwa mkuki, ikatoka damu na maji, ndipo zilipozaliwa sakramenti za kanisa. Aidha, tukio la askari wa Kirumi kumchoma Yesu na damu na maji kutoka lina maana nyingine kubwa katika maisha yetu. Hapo ndipo Ukristo ulipozaliwa; na ni kwa sababu hiyo mwanamke anapojifungua hutoa damu na maji kutokana na kupasuka kwa utando wa mfuko wa uzazi. Kutokana na hayo, Wakristo wanapoabudu msalaba wanaeleza umuhimu wa matukio na mafundisho waliyopata kupitia mateso aliyopata kiongozi wao na kuwa, msalaba ni chombo cha ukombozi.”
Enock Maregesi

Seth Dickinson
“If the Masquerade could not be stopped by spear or treaty, she would change it from within.”
Seth Dickinson, The Traitor Baru Cormorant

Brandon Sanderson
“It's interesting that the woman who wrote that treatise – the one you all practically worship in Alethkar –decided that all of the feminine tasks involve sitting around having fun while all the masculine ones involve finding someone to stick a spear in you. Telling, eh?”
Brandon Sanderson, Words of Radiance

Madeline Miller
“The spear that I do not see comes from behind. It pierces the skin of my back, breaks again to air beneath my ribs. I stumble, driven forward by the blow's force, by the shock of tearing pain and the burning numbness in my belly. I feel a tug, and the spear-point is gone. The blood gushes hot on my chilled skin. I think I scream.”
Madeline Miller, The Song of Achilles

Peter V. Brett
“He feared no challenger face-to-face, but war was deception, as Khevat had taught him, and not all men fought their enemies with spear and fist.”
Peter V. Brett, The Desert Spear

Billy Graham
“Sin pierced the very heart of God. God felt every piercing nail and spear thrust. God felt the burning sun. God felt the mocking derision and the body blows.”
Billy Graham, Billy graham in quotes

George R.R. Martin
“Fish never climb out of the kettle and shove a spear through your belly.”
George R.R. Martin, A Dance with Dragons
tags: fish, spear

Enock Maregesi
“Yesu alipokuwa msalabani watu wengi walimzunguka. Askari wa Kirumi aliyekuwa na chongo, na mkuki, alikuwa na jukumu la kumtesa Yesu hadi kufa kwa amri ya Pilato. Yesu alipolia kwa sauti kuu, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?”, yule askari alikurupuka na kumwendea Yesu. Lakini Yesu alishakata roho. Kuthibitisha kama Yesu alishakata roho, askari alimchoma Yesu mkuki kwenye mbavu kwa nguvu zake zote. Mkuki huo ukamtoboa Yesu hadi upande wa pili, ukatoboa hata moyo wake. Askari alipochomoa mkuki, damu na maji viliruka na kupiga jicho lake bovu. Papo hapo askari akapona na kuona vizuri. Alipoona kweli amepona na kuona vizuri, askari alipiga kelele, alipiga magoti na kuomba Mungu amsamehe dhambi zake. Msamaha una nguvu kuliko dhambi. Askari huyo atakwenda mbinguni. Haijalishi umechukia watu kiasi gani. Haijalishi umetesa watu kiasi gani. Haijalishi umeua watu kiasi gani. Haijalishi umetenda dhambi kiasi gani. Mungu anachotaka kutoka kwako, tubu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kabla ya kukata roho mapigo ya kasi ya moyo aliyoyapata Yesu kutokana na mshtuko wa hipovolimia, pia yalisababisha maji kujikusanya katika vifuko vya maji au ute kandokando ya moyo na kandokando ya mapafu. Mkusanyiko huu wa maji kandokando ya moyo hujulikana kama ‘pericardial effusion’ na mkusanyiko wa maji kandokando ya mapafu hujulikana kama ‘pleural effusion’. Hii ndiyo maana baada ya Yesu kukata roho, na askari wa Kirumi kurusha mkuki katika ubavu wake, baada ya kutoboa mapafu na moyo, damu na maji vilitoka katika mbavu za Yesu kama Yohana alivyorekodi katika Injili yake. Mapafu ya Yesu na tumbo la Yesu vilijaa damu na maji. Mkuki ulivyotupwa maji yalitoka katika mapafu ya Yesu na katika tumbo la Yesu, na katika utando unaozunguka moyo wa Yesu, kutokana na kupasuka kwa moyo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Askari wa Kirumi alimchoma Yesu mkuki ili andiko litimie. Askari huyo ambaye Biblia haikumtaja jina kwa sababu zilizoko nje ya uwezo wetu, alivyoona kweli amepona na ameona alishuhudia, na ushuhuda wake ulitoka moyoni, ili nasi tupate kusadiki. Wauaji wa Kirumi walipoona kwamba wale wezi waliosulubiwa pamoja na Yesu walikuwa bado hawajakata roho, waliwavunja miguu ili washindwe kupumua na hivyo kuharakisha kifo chao. Kwa upande wa Yesu, waliona alishapoteza fahamu na labda alishafariki. Kuthibitisha hilo askari wa Kirumi alirusha mkuki, nao ukatoboa utando unaozunguka moyo wa Yesu na mapafu ya Yesu, na damu na maji kutoka. Lakini yote hayo yalishatabiriwa miaka mingi kabla ya Yesu: ‘Hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa’ na ‘Nao watamtazama yeye ambaye walimchoma’.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kuna sababu za msingi na za kinabii za damu na maji vilivyotoka katika mbavu za Yesu Kristo msalabani. Ubavu wake uliochomwa na mkuki ulithibitisha kifo chake cha kibinadamu, huku vingine vyote vikitimiza unabii wake uliotajwa na Yohana.”
Enock Maregesi

“The sky fell on my head. Night invaded the bright afternoon. I suddenly felt as though a thousand iron spears pierced through my skin. I had never felt anything like that before.”
Tshetrim Tharchen, A Play of the Cosmos: Script of the Stars

Laurence Galian
“A deity is worshipped and adored with intense devotion and faith not only throughout South India and Sri Lanka but also in places such as Mauritius and Malaysia where there is a high population of Tamil people. The deity carries a sword of Light. This deity’s name is Lord Muruga. Muruga is the powerful son of Shiva and Shakti, the Mother and Father of the universe. They created Him from the elements of divine fire and holy water. He is the embodiment of bravery, wielder of spear of tremendous shining light, called the vel. This sacred spear destroys all negativity and fear in an instant.”
Laurence Galian, The Sun at Midnight: The Revealed Mysteries of the Ahlul Bayt Sufis

Alexandra Monir
“Outside the closed doors to the throne room, Sharif the high elder waited, holding a kaftan robe of red silk and velvet in one hand and a long spear nearly twice his height in the other. Jasmine's heart beat faster as she recognized the gold trim and signature jewels lining the robe, the ancient craftsmanship of the spear. These had belonged to Cyrus the Great, the first ruler of the empire. And in mere moments, she would be the first woman to feel them against her skin.
Nadia untied Jasmine's peacock cape while the high elder held out the red robe.
"Today you shed the persona of Jasmine, the princess," he said, "and step into the skin of a sultana."
Jasmine took a deep breath, slipping her arms into the preserved silk. The material was more fragile than anything she'd worn before, and she was conscious that one wrong step, one tear of the fabric, would be rip through history. Yet she felt stronger in the cape too, as though Cyrus were transferring his power through it to her. When Sharif handed her Cyrus's spear, she could barely contain her awe.”
Alexandra Monir, Realm of Wonders