Helikopta Quotes
Quotes tagged as "helikopta"
Showing 1-3 of 3
“Saa nane za usiku timu nzima ya Vijana wa Tume ilirudi San Ángel katika helikopta ya DEA, tayari kwa safari ya Salina Cruz katika jimbo la Oaxaca. Kukamatwa kwa Gortari, Eduardo na Dongyang ulikuwa ushindi mkubwa wa kwanza wa Tume ya Dunia. Ushindi huo ukalipua wimbi la kukamatwa kwa wahalifu wa kimataifa, wa Kolonia Santita, dunia nzima.”
― Kolonia Santita
― Kolonia Santita
“Vijana wa Tume walipofika kambini chini ya ulinzi mkali wakiwa na Kahima, polisi wengi walionekana kuwapigia saluti lakini wakubwa wao wakawakataza na kuwambia wao walikuwa watu wa kawaida kama wao. Walisindikizwa na lundo la polisi mpaka ndani ya jumba la utawala Murphy alimokuwa ameuhifadhi mwili wa Radia. Walipofika walishtuka, na hata kuwashangaza polisi. Mwili wa Radia haukuwepo! Walitafuta kila sehemu, na kuwambia polisi wawasaidie kutafuta, lakini Radia alishapotea. Murphy alipata wazo na kutoka nje, kwa kukimbia, polisi wengi wakimfuata; mpaka katika helikopta ya DEA ambapo alifungua mlango na kuingia ndani. Ndani ya helikopta hakukuwa na mtu!”
― Kolonia Santita
― Kolonia Santita
“Radia Hosni alikuwa na bahati kuliko watu wote duniani. Frederik Mogens alipofika katika helikopta na kukuta Murphy na Yehuda wakihangaika kuutafuta mwili wa Radia, hakushangazwa na walichomwambia. Kwa sababu alijua nini kilitokea. Radia alikutwa akipumua kwa mbali. Hivyo, Debbie na marubani walimchukua na kumpeleka Mexico City haraka ilivyowezekana. Black Hawk waliyokuwa wakiishangaa ilikuwa ya DEA. Lakini si ile waliyokwenda nayo Oaxaca. Ilikuwa nyingine ya DEA, iliyotumwa na Randall Ortega kuwachukua Vijana wa Tume na kuwapeleka Mexico City haraka ilivyowezekana. Black Hawk waliyokwenda nayo Oaxaca ndiyo iliyomchukua Radia na Debbie na kuwapeleka Altamirano (hospitali ya tume) mjini Mexico City. Mogens angekwenda pia na akina Debbie; lakini alibaki kwa ajili ya kumlinda El Tigre, na mizigo yake, na baadhi ya makamanda wake wachache. El Tigre angeweza kutoroka kama angebaki na polisi peke yao, na Mogens hakutaka kufanya makosa.”
― Kolonia Santita
― Kolonia Santita
All Quotes
|
My Quotes
|
Add A Quote
Browse By Tag
- Love Quotes 97.5k
- Life Quotes 76k
- Inspirational Quotes 72.5k
- Humor Quotes 43.5k
- Philosophy Quotes 29.5k
- Inspirational Quotes Quotes 27k
- God Quotes 26k
- Wisdom Quotes 23.5k
- Truth Quotes 23.5k
- Romance Quotes 23k
- Poetry Quotes 22k
- Death Quotes 20k
- Happiness Quotes 18.5k
- Life Lessons Quotes 18.5k
- Hope Quotes 18k
- Faith Quotes 18k
- Quotes Quotes 16.5k
- Inspiration Quotes 16.5k
- Spirituality Quotes 15k
- Religion Quotes 15k
- Motivational Quotes 15k
- Writing Quotes 14.5k
- Relationships Quotes 14.5k
- Life Quotes Quotes 14k
- Love Quotes Quotes 14k
- Success Quotes 13.5k
- Time Quotes 12.5k
- Motivation Quotes 12k
- Science Quotes 11.5k
- Knowledge Quotes 11k