,

Silaha Quotes

Quotes tagged as "silaha" Showing 1-4 of 4
Enock Maregesi
“Ndani ya kibweta cha risasi kuna vitu vitano vyenye uwezo wa kulipuka kama vile risasi, kasha, baruti, kitako na fataki. Risasi hutumika kama kombora – kitu kinachoweza kusafiri hewani na kulipuka baada au kabla ya kugonga shabaha – wakati kasha kazi yake ni kuhifadhi vitu vyote vya kibweta kwa pamoja kusudi visisambae. Baruti inayotoa au isiyotoa moshi ni poda yenye uwezo wa kulipuka ambayo ndani yake kuna mkaa, salfa na shura; ambayo husukuma kombora mbele kwa nguvu kubwa baada ya fataki kulipuka kupitia katika kitako cha kibweta. Kitako cha kibweta hutumika kama kiziduo cha risasi kutoka katika chemba ya silaha, wakati fataki kazi yake ni kuwashia baruti.”
Enock Maregesi

Julius Nyerere
“Moyo kabla ya silaha”
Julius Nyerere

Enock Maregesi
“Silaha kuu ya uchoyo ni kujitolea kwa ajili ya watu wengine. Ni upendo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Shetani hataacha kukuandama. Atakuandama mpaka siku utakapookoka. Yaani, siku utakapookolewa na Yesu Kristo, siku ambapo Shetani hatakuwepo tena. Silaha kuu tunayotakiwa kuwa nayo ni imani. Mungu hababaishwi na matatizo yako. Anababaishwa na imani yako.”
Enock Maregesi